To save content items to your account,
please confirm that you agree to abide by our usage policies.
If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account.
Find out more about saving content to .
To save content items to your Kindle, first ensure no-reply@cambridge.org
is added to your Approved Personal Document E-mail List under your Personal Document Settings
on the Manage Your Content and Devices page of your Amazon account. Then enter the ‘name’ part
of your Kindle email address below.
Find out more about saving to your Kindle.
Note you can select to save to either the @free.kindle.com or @kindle.com variations.
‘@free.kindle.com’ emails are free but can only be saved to your device when it is connected to wi-fi.
‘@kindle.com’ emails can be delivered even when you are not connected to wi-fi, but note that service fees apply.
Raia ni mtu aliyejiunga na watu kwa masharti fulani. Asitawisha maisha yake miongoni mwa watu, na watu wenyewe wasitawi kwa sababu ya kazi bora za raia huyo. Mndorobo ajifichaye mwituni hawezi kuitwa raia.
Sisi sote twataka watu wetu wasitawi, lakini hili hutegemea maendeleo ya kila raia. Mtu akiwa katika hofu ya mauti au ya hasara ya mali daima, hawezi kusitawisha ubora wake. Hali kadhalika kila raia akitenda apendavyo, patakuwa na machafuko na fujo kati ya watu. Hivyo kwa ajili ya usitawi wa kila mtu, na ule wa watu wote, raia hupewa haki fulani na baadhi ya kazi zikalazimishwa juu yake.
Raia hufaidi haki za hiari na za sheria. Ana hiari ya kufuata dini yoyote na kujifunza lugha yoyote. Raia akifikiri serikali haitendi vema, aweza kusema. Haki ya salama ya maisha na mali ni haki ya halali kwa wote. Serikali yapasa kulinda maisha na mali yetu. Raia ana haki ya kwenda popote apendako, kuanzisha kazi yoyote atamaniyo, kuoana na mtu yeyote aliye kufu yake na kuhudhuria mkutano wowote usiokuwa faraghani. Katika miliki za Kiingereza raia ana haki ya kuvota.
Kama pana haki za kufaidi, pana kazi za kutendwa vile vile. Uraia husisitiza mno kazi kuliko haki. Kazi zenyewe ni za hiari au sheria. Raia lazima atii sheria; kama hafanyi hivyo, huadhibiwa. Uaminifu serikalini ni kazi nyingine za raia. Lazima atumike katika nyakati za vita na lazima asaidie idara za serikali kama Polisi na nyingine. Ingawa haipendezi lakini ni kazi ya wajibu kwa raia kulipa kodi. Raia wengi wakiepa kulipa kodi serikali haiwezi kufanya kazi. Zaidi ya yote ni kazi ya kila raia mwaminifu kudadisidadisi, na kama hapana budi, kuonya serikali au watu akiona wanakwenda kinyume.
Haki na kazi hazijitegemei ila hutegemeana. Nidaipo kwamba mtu asiniue, hufasirika kwamba nisiue mtu. Kama kila mtu angaling’ang’ania haki zake mwenyewe lakini akaacha kuwatendea kazi wengine, pangalikuwa hapana haki iliyobaki kwa mtu yeyote mara moja.
Kusudi la haki na kazi za raia ni kusitawisha hali ya watu. Raia awapo mwaminifu katika kutenda kazi zake kama atakavyo sana kufaidi haki zake, nchi huwa imara huwa na umoja.
Kuna methali isemayo, “Akili razini ni afya mwilini.” Twaambiwa waziwazi na methali hii kwamba lazima tuwe na mazoezi ya mwili na mchezo, nasi twaonywa kwamba tusitupe mwili ukaharibika kwa sababu ya kusitawisha akili. Twaweza kuwa na akili razini kama tuna mwili wa afya tu.
Kwa desturi watu wote huzaliwa na mwili wa afya, lakini baadaye kwa sababu ya desturi mbaya au kwa sababu ya ukosefu wa sulubu ya kiwiliwili, mwili huanza kuharibika. Ni dhahiri kwamba kitu kisipotumiwa, huoza. Kukomesha uharibifu huu, mwili lazima uzoezwe kila siku katika namna fulani ya sulubu ya mwili. Njia bora ni kwamba kazi zetu lazima ziwe na sulubu ya mwili, kama tuonavyo katika maisha ya mkulima, mhunzi au hamali.
Kwa sababu hii twaona kwamba mazoezi ya mwili yametiliwa mkazo mwingi sana katika idara zetu za elimu. Kusoma si kazi nyepesi. Hakutumii akili tu lakini mwili hutumiwa vile vile. Kama vyuo havisisitizi mazoezi ya mwili hapana shaka wanafunzi wake watakonda na kuwa magofu. Wanafunzi wengi wangeonekana wamezeeka kabla ya wakati wao. Wangekuwa na sura za kusawajika na miili dhaifu. Ni jambo la maana sana kulazimisha mazoezi ya mwili katika vyuo, kwa sababu wakati wa ujana ndiyo wakati wa kuweka msingi wa afya mwilini. Hakika kubwa ya jambo hili inapatikana katika methali nyingine maarufu isemayo kwamba “udongo upate ungali maji”.
Haikaidiki kwamba mazoezi ya mwili ya lazima huchukiza kwa wanafunzi mwanzoni. Husemwa kwamba nusu saa ya kuchezesha mikono na miguu nje haina manufaa kwa mtu yeyote, kwamba hufaa kwa onyesho na kwamba ni kupoteza wakati bure. Lakini fikira kidogo huonyesha kwamba ina manufaa mengi sana. Ingawa nusu saa ya mara moja au mara mbili kwa juma moja haileti faida papo kwa papo kwa mwanafunzi, lakini hufumbua macho yake aone faida za mazoezi ya mwili. Mazoezi ya mwili ni mwongozo na onyo kama mafundisho mengine yafundishwayo katika vyuo vya elimu.
Methali hii nyepesi lakini maarufu sana. Mamoja kwa sababu ya wepesi wake, tusiidharau.
Ni jambo lijulikanalo na watu wote kwamba ukuta wa nyumba upasukapo, lazima tuuzibe upesi. Tusipofanya hivyo mapema ufa utazidi nao utahitaji kazi kubwa ya kuutengeneza. Pengine ukuta huweza kufanya ufa mkubwa sana, hata ni vigumu sana kuutengeneza. Kweli iliyo juu ya ukuta ni kweli juu ya nguo, viatu, magunia, madaraja, meli na vingine. Dosari ndogo katika vitu kama hivi lazima zitengenezwe mapema.
Methali hii huweza kutumiwa kwa mambo mbalimbali ya maisha. Mtu akipatwa na ugonjwa, asiudharau, lakini amshauri upesi mganga. Hili litamwepusha na maumivu mengi ya wakati ujao na uharibifu wa fedha. Akidharau, ugonjwa waweza kuwa hauponyeki ukamtia katika mauti.
Dosari ndogo katika eropleni, mashine kubwa na magudi lazima zitengenezwe mapema, kama sivyo hazitatengenezeka.
Methali hii husema lazima tufanye kazi yetu kwa kawaida. Mwanafunzi akisoma masomo yake kwa kawaida, hufaulu kwa urahisi. Lakini akiacha masomo yake akajikalia bure, atajiona amezongwa na mashaka makubwa ya masomo. Yamkini hata kwa bidii zake, ataona shida kufanikiwa.
Tabia mbaya lazima zikomeshwe mwanzoni vile vile. Wazazi au walimu wakiona watoto wadogo wavivu au fedhuli, lazima wakanywe. Wizi wa kalamu au mpira wa kufutia ni neno dogo. Lakini lazima lizuiwe mapema. Kama sivyo mtoto aweza kuwa mwizi mkubwa. Watu wengi hunywa ulevi ili kujiburudisha, lakini ulevi huwalafua mara moja wakawa walevi wakubwa. Kwa hivyo tabia mbaya kama hizo lazima zikomeshwe mwanzoni.
Twaonywa na methali hii kwamba tusidharau madogo. Pengine madogo huwa makubwa yakazaa matata mengi. Imesemwa kweli kwamba “Ufa huzamisha merikebu.”
Hivi karibuni nimeanza kupenda magazeti, na katika magazeti yote napenda sana “Mambo Leo.” Kwa hiyo baba yangu huninunulia kila mwezi. Kusema kweli, kama sipati gazeti hili mwisho wa mwezi najiona sina furaha. Lina mambo mengi mema hata laweza mara moja kuwa kipenzi kwa mtu yeyote alisomaye.
Mara nipatapo gazeti hili macho yangu hutazama maandiko makubwa katika ukurasa wa kwanza. Maandiko hayo hufunua habari muhimu za serikali. Kisha nasoma yafuatayo chini yake. Nikiona yapendeza nasoma mpaka mwisho.
Hili likiisha nasoma habari za nchi ngeni. Mambo muhimu sana hupata kutokea hapa yanayohusiana na ulimwengu na nchi yangu, kama biashara na mengine. Baadhi ya watu mashuhuri wa serikali au nchi mbalimbali husimuliwa hapa kwa ufasaha. Kwa ufupi nasema sehemu hii ndiyo nzuri katika gazeti nipendalo.
Kiu yangu ya ujasiri huzimwa mara moja na habari za safari za Sir Edward Twining, Gavana wa nchi yangu. Huwa kama nimerogwa nisomapo hotuba alizotoa katika majimbo na wilaya mbalimbali wakati wa safari zake. Sehemu hii haizimi kiu yangu tu lakini naona taarifa yake yote ina mambo muhimu sana. Hapa mvua imenyesha, pale jua kali, huku mazao yamevunwa, na huko yameharibika. Karibu habari za miji na vijiji vyote hupatikana katika sehemu hii. Habari kama hizo hunizima kiu zikanikomesha njaa.
Katikati ya gazeti hili hutokea picha nzuri za wenyeji mashuhuri au mambo makubwa. Maelezo chini ya picha hizi rahisi sana kufahamika. Ndugu zangu hucheka sana ninapowaeleza ni za kina nani au kitu gani.
Tena, makala juu ya mambo ya Serikali Kuu na tawala za wenyeji hupigwa chapa katika gazeti hili mara kwa mara. Makala haya yana masomo mazuri sana, na ingawa sina nafasi ya kusoma yote, lakini kila nipatapo nafasi ya kusoma hunipendeza sana. Kisha nasoma habari za michezo na mashindano yake.
Ukurasa wa mwisho una mashairi. Huu huchukuwa wakati wangu mwingi kwa sababu katika kazi zote za maandiko, mashairi yamenivuta kabisa. Hunifurahisha kuyasoma na kuyakariri. Yana uzuri wa ajabu katika mpango, lugha na fikira iliyo ndani yake.
2. Matumizi ya methali hii katika mambo mengine ya maisha
3. Methali yenyewe yasemaje
4. Tusidharau kutahadhari
5. Sura mbaya kwa nje
Tamthili ya methali zote methali hii ni matokeo ya maarifa barabara.
Dhahabu ni madini bora ing’aayo. Lakini kwa hili hatuwezi kusema kwamba kila king’aacho ni dhahabu. Kitu king’aacho huweza kuwa dhahabu au huweza kuwa si dhahabu. Methali hii yasema kwamba tusifikiri vitu vyote ving’aavyo kuwa dhahabu. Kuna madini zing’aazo kama dhahabu lakini hazina maana. Shaba iliyokwatuliwa, madini zilizoghushiwa na dhahabu za kuiga hung’aa kama dhahabu; lakini si dhahabu. Mng’ao wa madini una hadaa mara kwa mara, hivyo tungeangalia sana katika kupambanua dhahabu na shaba, madini zote mbili zing’aapo.
Methali hii husema kweli katika mambo mengine ya maisha. Kuna watu wengi waonekanao kuwa wastaarabu na bora. Lakini kwa kweli ni maayari. Waweza kudhani mtu aliyevaa libasi nzuri kuwa tajiri; lakini kwa kweli aweza kuwa maskini. Katika nguo vile vile hariri ya kuiga hufanana na hariri halisi, na kama hatuangalii, twapunjwa. Ukinunua kitabu kwa sababu kina jalada zuri tu, utajuta mara moja. Katika sanaa vile vile, sanaa zisizo maana huonekana mara kwa mara nzuri kama sanaa hasa. Lakini lazima tupambanue baina ya vitu hivi viwili. Hali hii hii imo katika vitu vya chakula. Uto wa nyama hufanana sana na samli safi. Basi kama huangalii, mfanyabiashara hukupunja kwa kukupa uto wa nyama kwa kukutoza thamani ya samli.
Methali yenyewe yasema kwamba sura huhadaa mara kwa mara. Kwa hivi tusitegemee sura nzuri tupu, lakini lazima tujaribu kugundua ubora wa watu au vitu. Yatuonya kuangalia katika kupambanua chema na kibaya, dhahabu na shaba na nafaka na kapi. Kama hatuangalii katika jambo hili, itatupasa kujutia uchaguzi wetu mbaya.
Lazima tutie sana maanani methali hii, lakini tusikithiri kujihadhari. Ingawa vyote ving’aavyo si dhahabu, vyote ving’aavyo si shaba. Kwa hivi tusituhumu kila kitu king’aacho. Kama uzembe katika kupambanua vitu au watu ni kosa, kukithiri kujihadhari katika jambo ni kosa vile vile. Tukituhumu mara kwa mara ubora wa mtu au kitu, maendeleo yetu yatakoma. Maisha yametegemea tumaini na uthabiti. Hivyo tusidhani mtu yeyote au kitu chochote kuwa hakina maana mwanzoni.
I am grateful to all the authors who contributed thoughtful reflections on my 2016 and 2023 articles; and to the editors of Africa for calling on me to have the last word and write back in a compelling conversation on knowledge production and the crisis of public universities in Africa. It is time to pull the strings together. As I seek to do this, my aim is less to answer – collectively or individually – the authors and their contributions to my articles. Rather, I endeavour to put on record further thoughts on issues about which I have been silent in earlier publications. In pursuit of a longstanding interest in (1) how knowledge is produced on non-metropolitan societies, (2) the future directions of postcolonial universities, and (3) the relations of knowledge and power in Africa, I ask further questions and examine new archives and bodies of evidence. I appreciate the difficulty of ignoring the economic determinants of Africa’s material base – built as it is on dependent and disarticulated capitalist economies. In recounting my lived experience as an eyewitness to university life in Africa, and in shedding more light on the historical problems that I grapple with, I acknowledge change and continuity in historical explanations and the historiographies of my universe. In the present as in the past, the sense of sight shapes experience. I admit, with Ludmilla Jordanova (2012: 3), that vision has a history and that objects necessarily play a central role within it.1 As Peter Burke (2008) has shown, looking at alternative evidence and records enables one to examine historical problems and subjects in a different and hopefully renewed way. Historians therefore ask different and new questions. Such questions are informed by the changing nature of the environments and universes of analysis, historiography and historical scholarship. These activities demand continuous examination of existing arguments and conclusions against the backdrop of changing evidence and facts. Understood as the best intellectual imagery of modern society, I turn to the postcolonial universities in Africa. Ultimately, this effort, together with my other works, should illuminate what one might safely conjecture about the future of the universities in Africa.
Nilizaliwa na nasaba bora. Mbingu ni baba yangu na Ardhi ni mama yangu. Tangu utotoni mchana nimevaa nuru na usiku nimejifunika giza. Kinyume cha viumbe wengine, nala kwa miguu badala ya kinywa. Hii ndiyo desturi yetu sisi miti. Kinywa hutumika kwa kusema tu kama kifanyavyo leo kwa kusimulia hadithi ya maisha yangu. Mtaona ajabu, lakini ndivyo nilivyoumbwa. Nami najivuna kama wajivunavyo viumbe wengine.
Nilianza maisha yangu miaka thelathini iliyopita. Huu si umri mkubwa kwa mti. Lakini ni mkubwa wa kutosha mkisikia mambo yaliyonipata. Nilipokuwa na umri wa miaka mitano mvua haikupatikana, Watu walianza kudhikika, nami nikakaribia kufa.
Umri wangu ulipokuwa miaka kumi palitokea dhoruba kali sana. Miti iling’oka, na nyumba kadha wa kadha zikaharibika. Mimi peke yangu ndiye niliyejizuia kwa nguvu zangu zote. Kusema kinaganaga, niliokoka kufa tu, si majeraha. Tawi langu moja lilivunjika nikaona uchungu mwingi sana. Wakati tawi lilipokuwa likianguka, lilipiga nyati aliyekuwa chini ya kivuli changu, watu wakapata nyama ya kula. Tukio hili liliamsha ushirikina wa watu tangu siku ile. Mtu mmoja aliyezoea kuabudu mizimu, alianza kuniabudu maana mti aliokuwa akiabudu kwanza ulikuwa umekwishang’oka.
Kwa kumfuata mtu huyu, watu wengine walianza kuniabudu vile vile, sijui kwa nini. Mwaka uliofuata matukio hayo mvua nyingi ilinyesha watu wakafurahi sana. Baadhi yao waliamini kwamba mvua ile ililetwa na ibada yangu nikafanywa mzimu mkubwa. Katika mwaka wangu wa kumi na tano palikuja hatibu mkubwa sana mjini kivuli changu kikachaguliwa kuwa mahali pa mazungumzo ya dini. Watu wa pande zote walikuja nikawa mahali pa haji kama Yeruselemi na Makka.
Tamasha kubwa za dini zilifanywa chini yangu nikawa katika utukufu kwa muda wa miaka kumi na mitano mfululizo. Kisha mambo yaligeuka. Siku moja watoto walikuwa wakicheza bui katika mti uliokuwa karibu na mimi. Walikuja kwangu wakaanza kucheza mchezo huo huo katika matawi yangu. Watoto kumi walisimama juu ya tawi moja. Tawi lilivunjika kwa sababu ya uzito wao; watoto wawili katika hao wakafa. Watu walichukizwa na tukio hili lakini waliendelea kuniabudu. Palikuwa na shida ya mvua katika mwaka huo huo. Na baya kuliko yote, ilikuwa ni ajali ile iliyotokea kwa watoto wale wawili. Tangu siku ile watu walinituhumu kwamba mashetani waovu walikuwa katika shina langu.
Husemwa kwamba milima huonekana mizuri kwa mbali. Hili ndiyo kusema kuwa milima huonekana mibaya tuikaribiapo? Yaweza kuwa kweli kwamba milima ni mkusanyo wa mawe na vumbi na misitu na miti. Milima ni sanaa moja katika sanaa nzuri kabisa za Maumbile. Hupendeza kutazama na kupanda. Furaha ya kupanda milima kubwa sana. Mtu huanguka akatoka damu kisha hupanda tena, lakini katika haya yote ipo furaha. Kwa furaha hii watu wengi wamefanya majaribu ya hatari kabisa ya kukwea vilele virefu vya milima. Majaribu mengi yamefanywa ya kupanda kilele cha Kilimanjaro, mlima mkubwa sana wa Afrika, na japo watu wadogo kama sisi hatuwezi kutenda ujasiri mkubwa kama huo, twaweza kupata fungu letu la furaha kwa kupanda kilima kilicho karibu yetu.
Zaidi ya kutupa furaha hii, milima hufaa sana. Ni ukuta imara kwa mashambulio ya adui. Hutukinga na tufani au pepo za baridi zitokazo upande mwingine. Milima mingine mirefu sana. Theluji huganda mara kwa mara juu ya vilele vyake. Hivyo hewa ya joto huburudika upepo mzuri ukapepea nyandani. Katika kiangazi, kwa sababu ya hali ya jua, theluji huyeyuka ikatiririka kingoni mwa milima hiyo. Milima hutupatia hifadhi, hewa ya kuburudisha na maji. Hufanya mito mikubwa. Hutupa madini mengi, aina mbalimbali za matunda, mimea ya dawa na miti.
Kando ya milima huota misitu mikubwa. Misitu hii ni makao ya wanyama waletao katika Afrika Mashariki wawinda wa nchi mbalimbali. Twapata ngozi, pembe na meno. Tunu hizi huongeza utajiri wa nchi. Wanyama katika msitu ni akiba kubwa ya chakula. Wandorobo huishi kwa chakula hiki. Hupatikana mapango ya ibada milimani vile vile.
Husadikiwa kwamba milima huimarisha ardhi, yamkini kwa sababu hii, yasemwa milima haikutani. Haiachi kazi yake hata kidogo ikakutana kwa maongezi ya uvivu. Mambo kama haya ya maumbile hutatiza akili ya mwanadamu.
Shani moja katika shani bora kabisa ulimwenguni ni mlima mrefu ukikaa vizuri chini, na kilele chake kiking’ara juu kwa nuru nzuri ya jua. Milima hutuongoza kuona utukufu, nguvu na uzuri wa ulimwengu.
KuanDika insha huonekana kugumu sana kwa wanafunzi. Sababu ya kuwa hivi ni ukosefu wa mwongozo mwema na ujasiri ndipo wanafunzi wengi Waafrika wakashindwa kuandika insha. Mwongozo kama huo haukosi kuwako kwa lugha ya Kiingereza bali haujawako kwa Kiswahili. Kwa manzili haya pana udhuru wa kutosha wa haja ya kuwako maonyo ambayo yatasaidia wanafunzi ambao bado hawajaweza kushinda mashaka ya Kiingereza.
1. Kusudi la kuandika insha.
Kusudi la kuweka uandishi wa insha katika oradha ya mafundisho ya chuoni lina maana mbili:
(1) Kujua kama mwanafunzi aweza kuwaza kidogo tena aweza kujenga mawazo yake vema na (2) kujua kama aweza kusema mawazo yake kwa ufupi na kwa lugha iliyo wazi na nyepesi kufahamika vizuri na kila mtu.
Si faida kwa mtu yeyote kujua neno ila aweze kulieleza kwa wengine. Dhahabu haina maana ikiwa katika ardhi. Kusudi la insha ni kushawishi au kuongoza; kuzungumza au kustarehesha; au kuandika makala ya kupiga chapa na kadhalika, ili ile dhababu iliyo katika moyo wake mtu ipate kuonekana.
2. Elimu ya kuandika insha.
Twakumbushwa taaluma ya kuandika kwa shairi maarufu la Pope lisemalo:
“Urahisi hasa wa kuandika huja kwa bidii, si bahati;
Na wachezaji bora ngomani ni wale ambao wamejidhatiti.”
Hapana elimu ipatikanayo pasipo taaluma, tena hususan ile ya kuandika insha. Bila ya shaka taaluma ya kuandika insha hutaka bidii; nayo huchosha mara kwa mara. Lakini yampasa mwanafunzi kuandika insha kadhaa kabla ya kuweza kuandika kwa wepesi. Ufasaha wa kuandika haupatikani kwa kusoma tu. Hana budi kujaribu kuiga waandishi mbalimbali kwa kuandika insha. Kwa taaluma ya kuandika peke yake ndipo awezapo kujua jinsi ya kutangua maneno yaliyo hafifu au yasiyofaa. Hata mpango wa mambo mbalimbali ya insha hupatikana kwa taaluma ya daima. Kwa maneno mengine, insha ni taaluma kwa waandishi kama ilivyo taburu kwa askari. Lazima mtu aandike insha nyingi kabla ya kuwa mwandishi mwema.
I want to say what a privilege it is to be invited to comment on Jeremiah Arowosegbe’s article ‘African universities and the challenge of postcolonial development’. First and foremost, this is because Arowosegbe’s piece is exactly the kind of intervention we need more of: passionately written, politically engaged commentaries on the state of African universities today by scholars based on the continent who are invested in charting the best way forward for their institutions. African universities have been in a kind of Janus-faced state for at least the last decade, if not longer. On the one hand, institutions with records of having been among the world’s most exciting universities of the 1960s and 1970s – Makerere, Ibadan, Dar es Salaam – have had to endure a near total, decades-long collapse driven by austerity programmes imposed by the International Monetary Fund (IMF) and forced on African states from the 1980s. This is a crisis that undoubtably lingers – indeed, Arowosegbe makes it his focus – and these universities have had to struggle not to be entirely defined by this story of lack and of failure. On the other hand, some of these institutions (including those named above) have come through the fire of this collapse and have emerged with new life that cannot be reduced to mere tendrils. On the contrary: the continent’s top dozen or so universities are today producing students who will very likely become the world’s next generation of humanists, social scientists and hard scientists focused on Africa, and beyond too. The pipeline for this present generation of students often now runs from undergraduate and master’s programmes in Africa, to top doctoral programmes in North America and Europe, to these students being the most competitive candidates for the mini-boom (relatively speaking) in tenure-track positions in disciplinary scholarship and pedagogy focused on Africa. Amidst a more general withering of the humanities in globally northern universities, African and Black Studies constitute a partial exception to the dying throes of higher education as we know it and are part of a laudable and long overdue diversification of the field. Adding to the reconfiguration of African Studies’ landscape of labour, the dramatic shortage of viable jobs in North America and the UK is making the job market for graduates of the world’s top PhD programmes a truly global one that includes Africa prominently. Not since the 1960s have we seen the prospect of top African universities being realistically able to attract new scholars trained in the global North to base themselves in Africa – a potential boon to African universities (even if one that remains more in potentia than realized).
Kwa neno zima uzalendo ni mapenzi ya nchi. Mapenzi haya hayafanyiki kwa njia za kubuniwa na watu lakini yamekwisha tangulia kuwa katika mioyo yetu. Uzalendo ni tabia ya maumbile, nasi tunayo toka wakati wa kuzaliwa. Twafikiri habari za nchi zetu kama tufikirivyo habari za baba na mama zetu. Adamu alitoka ardhini. Kwa hivi kila mtu hujali sana pahali alipozaliwa.
Baadhi ya watu hawakubali nao watayari siku zote kupinga pishi ya hoja zako kwa ukufi wa hoja zao. Wao hufikiri kwamba uzalendo ni maono ya ushupavu, na dalili ya uchache wa ustaarabu wa moyo. Kwao uzalendo ni imani ya kishenzi, kwa sababu hutenga kando nchi nyingine. Wadai kwamba mtu lazima apende ulimwengu mzima na watu wote wa dunia kama ndugu zake. Wazo la udugu wa ulimwengu hufanya kila mtu kuwa raia wa dunia si wa pahali pake padogo, pajulikanapo kama nchi yake. Lazima tuseme kweli kwamba wazo la udugu wa ulimwengu ni bora kwa makisio lakini kwa matumizi haliwezekani. Bora katika watu ni yule apendaye nchi yake kwanza. Pana mashaka makubwa kama mtu aweza kuwa amini katika mapenzi ya udugu wa ulimwengu bila kupenda nchi yake. Ikiwa hivyo, uzalendo huthubutisha ubora wa kupenda sehemu ya ulimwengu ambayo ndani yake tumezaliwa.
Mapenzi ya mtu ya nchi yake hayaonyeshi chuki ya nchi nyingine za ulimwengu. Uzalendo wa uongo ndiyo utufanyao kuchukia nchi nyingine. Aidha, lazima tupende nchi zetu kwa sababu ya nchi zenyewe. Pasiwe na kusudi baya au la choyo nyuma yake. Kuna uzalendo wa uongo vile vile ambao ni hila tufanyayo kwa makusudi yetu wenyewe ya choyo kwa sababu ya nia mbaya za kujitajirisha sisi wenyewe. Uzalendo wa kweli hutokana na mapenzi yasiyo choyo ya nchi zetu na heshima yetu ya historia na malezi. Uzalendo usitufanye kujiona kwamba sisi ni watu azizi ulimwenguni na makabila mengine yote si kitu.
Mapenzi ya nchi zetu huonekana kama maono bora, lakini hayana maana kama hayachukuani na matendo. Uzalendo wa matendo tu ndiyo wenye thamani yoyote nchi iwapo katika hatari ya shambulio la adui. Mapenzi ya mtu ya nchi yasiyo matendo yaweza kuwa mema katika nyakati za amani, lakini katika nyakati za vita uzalendo huthubutisha unyofu wake katika kitali.
Matumizi ya wastani na mawazo mema ni dalili za maisha ya furaha. Watu wakubwa wote wa ulimwengu wamesisitiza juu ya maisha ya wastani. Matumizi ya harija hufilisisha, hayasitawishi. Wazee wetu walikuwa watu wa wastani sana katika maisha. Walikuwa na haja chache lakini walikuwa na furaha. Walikaa mapangoni au katika vibanda vidogo, walivaa ngozi au mavazi ya wastani, wakala chakula cha kawaida. Walifurahi wakaridhika sana na maisha yao ya wastani. Lazima pawe na wastani katika mambo yote ya maisha. Mavazi yetu lazima yawe na wastani kwa kitambaa na kwa namna. Chakula chetu lazima kiwe cha wastani lakini kitie afya. Mapambo yetu lazima yawe ya faraja yasiwe ya fahari. Nyumba zetu zaweza kuwa za faraja lakini za wastani. Vitu vyote vya faraja lazima viwe vya wastani iwezekanavyo.
Tena yatupasa kujifunza wastani katika maadhimisho yetu. Twatumia mali yetu pasipo kuwaza katika maadhimisho ya arusi, katika chakula, nguo na sherehe. Tuna harija ya fedha wakati wa Idi au Sikukuu. Twamimina mifuko yetu kwa mazishi ya jamaa. Hili halifasiri kwamba hatupasi kujifurahisha kwa sababu njema.
Wastani hupingana na fahari na anasa. Twavaa mavazi ya siku hizi, si kwa sababu yatupa furaha kubwa, lakini kwa sababu wengine wapate tuajabia. Twaweka mapambo ya mitindo mipya kabisa katika nyumba zetu si kwa sababu ya faraja zaidi ila kwa kuonyesha utajiri wetu. Lakini hapana mwisho wa fahari na anasa. Kila tuzidipo kuzipata twazidi kuzitamani. Anasa na fahari hazituridhishi, lakini wastani hutupa amani mioyoni mwetu.
Wanawake hushindana kwa mavazi yao. Kanga, mabuibui, marinda, viatu, soksi, mifuko, miavuli, kofia na vingine hugeuzwa ajabu kwa mawazo ya wanawake. Pana mifano kwamba waume wapendapo wastani wake wao hupenda fahari. Wanawake lazima wajifunze ubora wa wastani.
Wastani hutupa furaha, lakini anasa hutupokonya. Wastani huleta amani moyoni, lakini fahari huifukuza. Wastani hutupa ridhaa, lakini anasa hutunyang’anya. Libasi ya urembo haizidishi furaha yetu hata chembe, ila pengine hupingana na mwendo wetu. Twalipa fedha nyingi kwa anasa zetu. Walakini, wastani kwa sababu ya wastani peke yake hutufurahisha. Hupunguza wakati, gharama na kazi ambayo huweza kutumiwa kwa usitawi wako mwenyewe, na kwa maendeleo ya nchi yako.
Wazo la watu wengi juu ya muungwana ni kuwa mtanashati, au labda, mtu arifu mwenye cheo kwa watu. Lakini nguo nzuri hazitukuzi mtu kuwa muungwana. Tamthili ya hili ni kwamba nguo ni kama ngozi ya mtu au mnyama; au hasa ni duni sana kuliko ngozi au manyoya. Ngozi ya simba haiwezi kufanya punda kuwa simba. Uungwana wa kufanywa na mshoni ni mzaha, si uungwana wa kweli. Neno muungwana lina maana kubwa zaidi kuliko nguo nzuri au adabu nzuri au elimu nzuri. Twatumia vibaya neno hili tulitumiapo kwa mtu yeyote aendaye kwa miguu miwili. Uungwana hauhusiani na kuzaliwa na watu bora, au utajiri au sura. Huhusiana na taamuli au maadili kadha wa kadha ya akili na wema.
Kwanza muungwana hawezi kuudhi wala kudhuru mtu kwa neno au tendo lake, au hata kwa tazamo lake. Ana moyo wa uvumilivu naye huweza kusikiliza kwa makini maono ya wengine, bila kujaribu kulazimisha maono yake kwao. Ni karimu, mnyofu na amini katika tabia yake kwa wengine. Hapendi kujionyesha alivyo tajiri au alivyoelimika. Kwa kweli, ajua werevu wa kuficha maadili yake mwenyewe. Hajisifu wala hapendi maono yake mwenyewe. Kwa hivyo, ni msikilizaji mwenye saburi kuliko msemaji ajisifuye mwenyewe. Tabia yake njema naye tayari kusaidia, lakini hana makuu wala unafiki. Mnyofu katika kila asemalo au atendalo. Hajisifu kwa matendo yake wala hadunishi matendo ya wengine kwa wivu. Hutakia wote heri wala hana undani na mtu hata mmoja.
Tamthili kama hii juu ya muungwana huweza kutia wazo la udhaifu moyoni. Lakini sivyo kabisa. Muungwana asipodhuru mtu yeyote, haionyeshi kwamba hana nguvu ya kufanya dhara. Haudhi wala hadhuru mtu yeyote, kwa sababu ajua kwamba ushenzi kama huo ni kinyume cha uungwana. Ajua heshima ya mtu naye humheshimu kama mtu.
Tabia yake njema kwa wageni na jamaa zake vile vile. Mwema kama baba, mwaminifu kama rafiki na msaidizi kama ndugu siku zote. Hutenda tena hujiendesha kama raia mwadilifu, ajuaye kazi na madaraka yake kwa watu. Huchukuana na watumishi wake kwa mapenzi, huruma na upole. Huheshimu heshima yake na kwa sababu hiyo huheshimu heshima ya wengine.
Hii ni methali ya hekima sana. Hutumika katika nchi zote na makabila yote. Katika kila pahali ulipo, methali hii ifanye kama hirizi yako au ngao ya mwili wako.
Hufaa hasa kwa afya. Yakupasa kutahadhari na ugonjwa. Haifai kuachilia ugonjwa ushambulie mwili wako na halafu kuuponya. Afadhali kujikaga ndui kwa kuchanja chale kuliko kufanya bidii ya kujiponya baada ya shambulio lake.
Serikali hushika methali hii nayo huzuia maambukizo kwa kudumisha hali ya usafi na kwa kuchanja watu. Kama isingeangalia, maambukizo yangetokea. Halafu kazi ya kuyakomesha ingekuwa ngumu mara nyingi sana kuliko kazi ya kuyazuia.
Methali hii hutumika kwa mambo mengine ya maisha vile vile. Heri kuepuka maovu kuliko kufikiri kutokana nayo baada ya kuyaingia. Afadhali kutahadhari kabisa na moto katika nyumba au chombo kuliko kungojea mpaka moto utokee ndipo uanze kuuzima. Wazee wenye busara hulea watoto wao vizuri; lakini wazee wajinga huachilia watoto wao watende watakalo, wakifikiri kwamba wataweza kuwarudi halafu. Basi, kwa kweli, marudi huwa na taabu kubwa sana baadaye. Serikali ikiachilia matendo ya uasi ya jamii au watu fulani mwanzoni, kwa matumaini ya kuyarudi halafu, ingekabiliwa na taabu mara moja.
Kuna methali nyingine zithibitishazo methali hii. “Fungato hainyong’onyezi mikono,” ina maana hii hii. Methali nyingine hutuonya kujenga nyumba tutie na mlango wa kufunga.
Hadhari haigharimu sana kuliko tiba. Hupunguza wakati na gharama. Hadhari nyepesi sana kuliko kujiponya. Wakati wa kufanya hadhari huna wasiwasi pia waweza kufanya mashauri yako polepole na vizuri. Mashaka ya kujiponya yakabilipo, mtu hufadhaika akafanya mambo kwa haraka. Hadhari haina maumivu; lakini kujiponya kuna maumivu mengi. Hadhari ina matumaini mengi sana kuliko kujiponya. Kago la kuchanja litazuia kabisa ndui; lakini mara shambulio la ndui likitokea, hapana ahadi ya kupona. Huweza kuleta hata mauti.
Kwa hivi kila mtu mwenye busara lazima atahadhari na magonjwa na mashaka. Maisha yetu machache sana. Hatuwezi kuwa na wakati mrefu wa kujiponya mara kwa mara. Kwa hivyo, “Tahadhari” ni neno la siri la kutujulisha habari za maisha yetu.
Kusudi la kitabu hiki ni kusaidia kama iwezekanavyo wanafunzi wa skuli katika kushinda mashaka ya kuandika insha. Si kikubwa cha kusifiwa, lakini si kidogo vile vile cha kuacha kuangaliwa na watu wengine watafutao mwongozo wa usanifu na vitabu. Kutunga na kuandika kuna mashaka mengi. Pasipo mwongozo ni watu wengi, ambao labda wengekuwa waandishi bora, hukata tamaa wakasema kwamba elimu hii imejaliwa watu wachache tu. Sivyo kabisa; kila elimu hupatikana kwa kujifunza na kujizoeza. Hapana madai yafanywayo na mwandishi wa kitabu hiki kwamba ukamilifu wote wa kuandika umo humu. Haiwezekani kueleza katika kitabu kidogo kama hiki namna zote za kuandika. Walakini, ingawaje hivyo, majaribio mbalimbali hutolewa yawezayo kuongoza katika jitihadi ya kukaribia au kufikia ukamilifu utakiwao. Yamkini kitakuwa na msaada kwa wanafunzi na wengine wenye ushawishi wa kusanii. Kwa hivi, kitabu hiki ni kimoja katika vitabu vilivyojaa mavuno ya fikira zisizokwisha ladha na uzuri.
Watu wengi hulia kwa sababu ya umaskini kama ni uovu mkubwa, na yaonekana kama imani ikubalikayo kwamba laiti wangalikuwa na fedha, wangekuwa na furaha na ubora tena wangepata mengi katika maisha. Kinyume chake ni kwamba, kwa desturi pana starehe kubwa katika vibanda duni vya maskini kuliko katika nyumba nzuri za matajiri. Nawasikitikia mara kwa mara wana na mabinti wa matajiri watumikiwao na mayaya wakawa na watumishi baadaye. Kwa sababu najua jinsi makao ya kimaskini yalivyo mema na yalivyo na ladha, furaha na usafi. Jinsi yalivyosalimika na hadhari ya mashaka, wivu na husuda za watu. Mambo haya ndiyo yanisikitishayo juu ya watoto wa matajiri nikashangilia watoto wa maskini. Kwa sababu hizi ndiyo maana miongoni mwa watu maskini huzuka mara kwa mara watu wengi wenye nguvu, mashuhuri na wajitegemeao wenyewe. Kama utasoma orodha ya watu wakumbukwao milele utaona kwamba wengi wao walipata baraka za kulelewa au kutunzwa katika chuo kikali cha umaskini.
Nchi ya ukulima kama Afrika Mashariki hutaabishwa na njaa mara kwa mara. Hili hutokea mazao yasipopatikana kwa sababu ya nzige na shida ya mvua. Nzige ni wadudu waharibifu sana kwa mimea. Mvua za kutangulia kabla ya wakati, zile za kuchelewa, kuuza mavuno yote na ukulima mdogo ni sababu nyingine ziongozazo sehemu nyingi za nchi hii katika njaa.
Mazao yasipopatikana, matajiri huficha vyakula, kwa hiyo bei zake hupanda. Watu maskini hawawezi kununua chakula kwa bei kubwa na kwa hiyo lazima wapunguze mahitaji yao.
Hali ya chakula huzidi kuwa mbaya kidogodogo. Njaa huenea pande zote, hutia ukiwa katika nchi ikakatisha watu tamaa. Wanawake na watoto wengi hulilia chakula, lakini hapana chakula cha kuwaokoa. Mwisho wengi wao hufa kwa njaa. Watu wengi hula majani na mizizi ya miti. Hata vitu hivi huadimika pia. Wengine hutafuta chakula katika majaa. Watu huenda huku na huko, hawaoni mtu hata mmoja wa kuwakaribisha ila njaa. Kwa hali hii watu hulilia chakula na mwisho wao wenyewe huwa chakula cha njaa.
Dhiki ya wanyama kama ng’ombe, kondoo, na mbuzi huzidi kuwa mbaya wakati misitu ya malisho ionekanapo kama jangwa. Hutangatanga huku na huko wakilia kutafuta takataka yoyote waonayo njiani. Kwa muda mdogo nchi hutapakaa magofu ya wanyama. Fikiri Wamasai ambao huishi kwa maziwa na nyama. Hali yao huwaje wakati huo.
Shida ya maji huzidisha hali kuwa mbaya mara kwa mara. Visima, maziwa na mito mingi hukauka. Wanadamu na wanyama hudhuriwa sana na kiu. Jitihadi hufanywa za kuleta maji toka nchi za karibu, lakini hayatoshi. Hapo hali ya wanyama huzidi kuwa mbaya pia.
Kwa desturi njaa hufuatana na majinai na maambukizo. Watu hufanya namna zote za majinai ili wapate chakula. Mapokeo ya watu wa Afrika husema kwamba njaa ilisaidia nusu ya biashara ya utumwa. Tena shida za chakula na maji huleta maambukizo kama kipindupindu, kuhara damu na kadha wa kadha.
Kwa kweli sasa njaa haina dhara kubwa kama ilivyokuwa zamani. Twashukuru majilio ya motakaa, reli, meli na eropleni maana chakula huwezekana kupelekwa upesi katika nchi zenye njaa.